Our Activities and Projects/Shuguli na Miradi ya UDT

Uwanji Development Trust (U.D.T) is a charitable, non-profit making, community-based trust. UDT was established in 2008 and became registered on 28th July 2010 by a certificate of registration no.S.A.16950 under society ordinance act 1954, society Act cap 337 (R.E.2002) of the United Republic of Tanzania. UDT is involved with several activities which include, but are not limited to, the following; 1.Promoting access and provision of quality education; 2. Provide assistance on health matters with special focus on HIV/AIDS; 3.Take measurable actions on the protection of environment; 4. Cooperate with governmental and non governmental stakeholders for technical and financial sustainable development issues and act as implementing agency; 5. Perform any other activity for the sustainable development of Uwanji people.
Join our cause by writing us: Our email address is udt2010[at]live.com or contact one of the following for more details; Chaiperson -Toba Nguvila - +255 755 097181. Deputy Chairperson - Rev. Naibu Nyambo +255 754 387364. Secretary - Valentine Malila - +255 755 474579. Deputy Secretary - Amani Mbwilo - +255 753 858527.

15 Feb 2013

MAELEZO YA MKUTANO MKUU WA MWAKA wa UDT

 

TAREHE YA MKUTANO

Mkutano utafanyika tar. 2/03/2013 siku ya Jumamosi


ENEO LA MKUTANO
Mkutano utafanyika mjini Matamba, ukumbi utatangazwa baadaye

NAMNA YA KUFIKA (kwa wenzetu ambao hawajafika Matamba siku nyingi  ni lazima tuwakumbushe namna ya kufika Matamba).

Kufika mkutanoni ni rahisi sana kwani kokote utakakotokea utashuka Chimala na kuna magari mengi sana ya kupandisha milimani, na kama bahati mbaya ukichelewa unaweza kuwasiliana na mratibu gari iliyopo Chimala ikakusubiria, Ikumbukwe ni mkutano wa Wawanji  hivyo kuna ushirikiano wa hali ya juu. 

Kama una usafiri binafsi, kwa kuwa ni kipindi cha mvua ukifika Chimala unaweza kuchagua njia ya kupita au Mfumbi au Ngoje kutokana na aina ya gari utakayokuwa umesafiri nayo, lakini njia kwa kiwango fulani zinapitika.

WASILIANA NA MRATIBU WA MKUTANO

Namba ya simu ya mratibu wa mkutano ni  +255 753900488, Tafadhali wasiliana naye kama utakuwa na swali ambalo halijibiwi na maelezo yaliyotolewa hapa.

MALAZI

Kwa kweli tunamshukuru sana Mungu kwani Matamba pana hoteli nzuri mpaka za kitalii na kama hujisikiii kulala hotelini Wawanji ni wakarimu sana utapata huduma ya malazi na chakula kutokana na utaratibu ambao viongozi wa mkutano watauandaa.

CHAKULA 

Chakula cha mchana siku ya mkutano kitatolewa, ndiyo maana tunawasisitiza wawanji kuhudhuria na kuchangia angalau Tsh.5000 kwa ajili ya vinywaji laini na chakula cha mchana. kama hutaweza kuhudhuria unaweza kutuma mchango wako kwa M-pesa kwa namba hizi. 0756-286018

TAFADHALI FIKA BILA KUKOSA KWA MAENDELEO YA UWANJI

Maelezo Mengine (kama ajenda za mkutano n.k) yatatolewa baadaye



No comments: